Monday, April 29, 2013

ITALIA KUPUNGUZA MISHAHARA YA MAWAZIRI

Waziri mkuu mpya wa Italia, Enrico Letta, amesema kuwa hatua ya kwanza kufanywa na serikali yake itakuwa ni kuondoa mishahara ya mawaziri ambao pia ni wabunge ambao kwa sasa wanapokea mishahara miwili. Akilihutubia bunge la Italia, Letta amesema katika kuonyesha mfano, serikali lazima ifute mishahara kwa mawaziri ambao pia ni wabunge. Hatua hiyo ni katika kujibu hasira ya wananchi wa Italia kuhusu wanasiasa wenye mishahara miwili wakati ambapo nchi hiyo inakabiliwa na matatizo ya kiuchumi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO