Monday, April 29, 2013

UGIRIKI YAPUNGUZA AJIRA 15,000

Bunge la Ugiriki limepitisha hatua zaidi ya kubana matumizi, ikiwemo kupunguza nafasi 15,000 za ajira ifikapo mwishoni mwa mwaka ujao wa 2014. Sheria hiyo pia imerefusha kodi ya mali kwa mwaka mmoja mwingine. Baada ya mjadala wa siku moja, serikali ya Ugiriki imepitisha sheria yenye kurasa 110 katika kifungu kimoja. Wakopeshaji wa kimataifa wa Ugiriki wanaitaka nchi hiyo ipunguze gharama zake kabla haijapatiwa msaada wa Euro bilioni 8.8 kwa ajili ya kuuokoa uchumi wake. Hata hivyo, wananchi wa Ugiriki wameingia mitaani kwenye mji mkuu wa Athens, kupinga hatua hiyo ya serikali ambayo ni ndogo kuliko ilivyotarajiwa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO