Tuesday, April 02, 2013

KARZAI ZIARANI MAREKANI


Rais Hamid Karzai wa Afghanistan anajaribu kuimarisha msimamo wa serikali yake kabla ya vikosi vya kimataifa kuondoka Afghanistan mwishoni mwa mwaka 2014. Rais Hamid Karzai wa Afghanistan ameondoka Kabul kuelekea Marekani ambako anatazamiwa kusalia kwa siku kadhaa.Amepangiwa kuzungumza na kiongozi mwenzake wa Marekani,Barack Obama kuhusu hali ya utulivu nchini mwake baada ya shughuli za kijeshi za vikosi vya kimataifa vinavyoongozwa na jumuia ya kujihami ya NATO zitakapomalizika mwishoni mwa mwaka 2014 na pia uchaguzi wa rais nchini Afghanistan.
Mada zote hizo mbili zina umuhimu mkubwa kwa mustakbali wa nchi hiyo.Idadi ya wanajeshi watakaosalia ni muhimu kwa usalama na uchaguzi utabainisha njia gani itafuatwa na nchi hiyo inayozongwa na mizozo. Mada nyengine zitahusiana na uchumi,uhusiano pamoja na nchi jirani na Afghanistan na hasa Pakistan na mazungumzo kuhusu uwezekano wa kufikiwa makubaliano ya usalama kati ya Marekani na Afghanistan.
Wataalam wanakadiria vikosi vya Marekani na jumuia ya kujihami ya NATO vitakavyosalia Afghanistan baada ya mwaka 2014,vinaweza kufikia wanajeshi elfu 30. Hata hivyo raia wengi wa afghanistan wanahofia,maeneo ya kusini na mashariki ya nchi hiyo yanayopakana na Pakistan,yanaweza kuangukia mikononi mwa waasi,mara baada ya vikosi vya kimataifa vinavyoongozwa na NATO-ISAF vitakapoihama nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO