Saturday, April 20, 2013

KURA ZA VENEZUELA KUHESABIWA TENA


Rais mteule wa Venezuela, Nicolas Maduro, leo amepata uungaji mkono wa viongozi wa mataifa ya Amerika ya Kusini  mjini Lima, kuhusiana na  mipango yake ya kutanuwa ukaguzi wa kura kwa njia ya elektroniki, kama njia ya kuituliza hali ya mambo kutokana na mzozo juu ya uchaguzi wa rais uliofanyika Jumapili iliopita. Hayo yanafuatia mkutano wa Umoja wa Mataifa ya Amerika ya Kusini, UNASUR, uliofanyika  kwenye mji mkuu wa Peru, Lima, masaa machache kabla ya mpango wa kuapishwa Maduro mjini Caracas. Maandamano ya upinzani yalizuka nchini Venezuela baada ya Maduro kushinda uchaguzi wa Jumapili kwa kiasi ya asilimia mbili zaidi ya kura za mpinzani wake Henrique Capriles ambaye amedai kura zihesabiwe upya. Tume ya Uchaguzi nchini humo sasa imesema itahesabu tena asilimia 46 ya kura iliyosalia, baada ya awali kuzihesabu tena zaidi ya nusu ya kura zilizopigwa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO