Thursday, May 30, 2013

MADAGASCAR YAAKHIRISHA TAREHE YA UCHAGUZI

Serikali ya Madagascar imetoa amri ya kuakhirishwa tarehe ya kufanyika uchaguzi wa Rais na Bunge nchini humo. Serikali ya mpito ya Madagascar jana ilitangaza kuwa, Baraza la Mawaziri limeafiki kuakhirisha tarehe ya uchaguzi wa Rais na Bunge baada ya kufanya vikao kadhaa vya kutafuta njia za kumaliza mgogoro wa kisiasa wa nchi hiyo.
Serikali ya Antananarivo aidha imesisitiza kuwa, tume ya uchaguzi ya Madagascar inawajibika kutayarisha jendwali la kuitisha uchaguzi huo kwa mujibu wa tarehe zitakazotangazwa tena.
Duru ya kwanza ya Uchaguzi wa Rais wa Madagascar ilikuwa imepangwa kufanyika Juni 24 na duru ya pili Septemba 25 mwaka huu pamoja na uchaguzi wa Bunge.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO