Monday, April 22, 2013

MISRI KUMHUKUMU NDUGU WA GHADAFI

Mwendesha mashtaka Mkuu nchini Misri, anakusudia kumpandisha kizimbani mtoto wa ndugu wa dikteta aliyeuawa nchini Libya Kanali Muammar Gaddafi. Ahmed GaddafAl-Dam atapandishwa katika mahakama kuu nchini Misri, kwa tuhuma za kuanzisha mauaji, kupambana na askari wa usalama na kumiliki silaha kinyume cha sheria. Itakumbuwa kuwa, tarehe 19 mwezi Machi mwaka huu, Ahmed GaddafAl-Dam aliwafyatulia risasi Polisi wa Kimataifa Interpol na wa Misri na kumjeruhi mmoja wao, katika oparesheni ya kumtia mbaroni mwana huyo wa ndugu wa Kanali Muammar Gaddafi. Mbali na idara ya mahakama nchini Misri kupinga kumkabidhi Ahmed GaddafAl-Dam kwa serikali ya Libya, imetangaza kumshitaki katika mahakama zake huku ikiwa tayari imekwishatekeleza usaili dhidi yake

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO