Mwendesha mashtaka Mkuu nchini Misri, anakusudia kumpandisha kizimbani mtoto wa 
ndugu wa dikteta aliyeuawa nchini Libya Kanali Muammar Gaddafi. Ahmed 
GaddafAl-Dam atapandishwa katika mahakama kuu nchini Misri, kwa tuhuma za 
kuanzisha mauaji, kupambana na askari wa usalama na kumiliki silaha kinyume cha 
sheria. Itakumbuwa kuwa, tarehe 19 mwezi Machi mwaka huu, Ahmed GaddafAl-Dam 
aliwafyatulia risasi Polisi wa Kimataifa Interpol na wa Misri na kumjeruhi mmoja 
wao, katika oparesheni ya kumtia mbaroni mwana huyo wa ndugu wa Kanali Muammar 
Gaddafi. Mbali na idara ya mahakama nchini Misri kupinga kumkabidhi Ahmed 
GaddafAl-Dam kwa serikali ya Libya, imetangaza kumshitaki katika mahakama zake 
huku ikiwa tayari imekwishatekeleza usaili dhidi yake
No comments:
Post a Comment
TUPE MAWAZO YAKO