Monday, April 22, 2013

POLISI 23 BRAZIL WAFUNGWA KIFUNGO CHA MAISHA

Duru za habari nchini Brazil zinaarifu kuwa, polisi 23 wa nchi hiyo wamehukumiwa adhabu ya kifungo cha maisha, kwa kosa la kuwaua wafungwa nchini humo. Kwa mujibu wa habari hiyo polisi hao waliohukumiwa kila mmoja kifungo cha miaka 156, walihusika katika mauaji makubwa zaidi dhidi ya wafungwa 111 katika jela moja ya nchi hiyo mnamo mwaka 1992. Aidha polisi hao 23 ni miongoni mwa polisi 26 ambao walihukumiwa hapo jana na kuachiliwa huru watatu kati yao. Maafisa hao wa polisi ambao wengi wao tayari walikuwa wamestaafu, walihusika katika mauaji ya wafungwa katika jela ya Carandiru iliyopo katika mji wa Sao Paulo mwaka huo uliotajwa. Hata hivyo mawakili wa polisi hao walioitaka mahakama ya Sao Paulo kuwapunguzia adhabu wateja wao, walidai mahakamani kuwa, polisi hao waliwafyatulia risasi wafungwa hao baada ya maisha yao kuwa hatarini.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO