Sunday, April 21, 2013

MURSI: USHIRIKIANO NA IRAN SI DHIDI YA NCHI NYINGINE

Rais Muhammad Mursi wa Misri amesema kuwa, siasa za nje za Cairo zinalindwa na maslahi yake ya taifa na kuongeza kuwa uhusiano wa nchi hiyo na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran si kwa madhara ya nchi nyingine yoyote ile. Akizungumza na kanali ya televisheni ya al Jazeera hapo jana, Rais Muhammad Mursi wa Misri amebainisha kuwa Iran ni moja ya nchi za Kiislamu duniani na kwamba wakati Misri inapokuwa na uhusiano na Iran, uhusiano huo hauwi dhidi ya nchi yoyote ile. Tehran ilikata uhusiano wake wa kidiplomasia na Misri baada ya Mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979 nchini Iran kufuatia hatua ya Cairo ya kusaini mkataba wa Camp David na utawala wa Kizayuni wa Israel na kumpa hifadhi Mohammad Reza Pahlavi mfalme aliyepinduliwa na wananchi hapa Iran. Hata hivyo uhusiano kati ya Tehran na Cairo umekuwa ukiboreka kufuatia mapinduzi ya wananchi wa Misri ya mwaka juzi yaliyomng'oa madarakani dikteta wa nchi hiyo Husni Mubarak.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO