Sunday, April 21, 2013

NAIBU MKUU WA HIZBULLAH ASEMA WAKO TAYARI KWA NJAMA ZOZOTE ZA ISRAEL NA MAREKANI


Naibu Mkuu wa Baraza la Utendaji la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza kwamba, harakati hiyo imejiandaa kikamilifu kwa ajili ya kukabiliana na njama za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Mashariki ya Kati. Sheikh Nabil Qaouq amesema kuwa, kuna haja ya kuendelezwa muqawama dhidi ya maadui na kwamba, muqawama ni dharura ya kitaifa na stratejia kwa ajili ya kukabiliana na vitisho vya utawala haramu wa Israel ambao unataka kuutumia vibaya mgogoro wa sasa wa Syria.
Sheikh Nabil Qaouq amesisitiza kwamba, katika hali ya hivi sasa Hizbullah iko katika hali nzuri kabisa ya maandalizi, jambo ambalo hata Ehud Barak, waziri wa zamani wa vita wa Israel amelikiri bayana. Naibu Mkuu wa Baraza la Utendaji la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon ameongeza kuwa, kama ambavyo muqawama ulipata ushindi mbele ya utawala wa Kizayuni wa Israel utazishinda pia njama za Marekani kwa kuitisha uchaguzi na kuunda serikali ya umoja wa kitaifa nchini Lebanon.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO