Saturday, April 20, 2013

MALI KUFANYA UCHAGUZI JULAI

Rais wa mpito wa Mali, Dioncounda Traore amewahakikishia washirika wa kimataifa kwamba nchi yake iko tayari kufanya uchaguzi wa kidemokrasia ifikapo mwezi Julai mwaka huu, kama alivyoahidi. Matamshi hayo ameyatoa kwenye mji mkuu wa Bamako, mwanzoni mwa mkutano wa wajumbe wa Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya, Umoja wa Afrika na Jumuiya ya Kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi-ECOWAS. Rais Traore amesema kutokana na msaada wa marafiki wa Mali, uchaguzi wa nchi hiyo utafanyika kwa muda uliopangwa. Amesema nchi hiyo inayopambana na waasi wenye itikadi kali za Kiislamu iko salama, ingawa bado juhudi zaidi zinahitajika kuimarisha usalama. Katika tamko lililotolewa mwishoni mwa mkutano huo, wajumbe wamefurahishwa na hatua ya kufanyika kwa uchaguzi wa urais mnamo Julai 7 na wa wabunge utakaofanyika Julai 21.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO