Monday, April 22, 2013

WAAFGHANISTAN WASIMAMIE WENYEWE UCHAGUZI WAO

Rais Hamid Karzai wa Afghanistan ametahadharisha juu ya uingiliaji wowote wa kigeni katika uchaguzi ujao wa rais nchini humo. Amesema wananchi wenyewe ndio wanaoapasa kuongoza mchakato wa uchaguzi ujao wa rais nchini humo. Rais Hamid Karzai aliyasema hayo jana katika mkutano wa baraza la usalama la serikali ya Afghanistan huko Kabul. Katika mkutano huo maafisa wa ngazi ya juu wa Afghanistan pia waliahidi kuwa uchaguzi ujao wa rais utakuwa huru na wa kiadilifu. Itakumbukwa kuwa Rais Hamid Karzai mwaka jana alisema kuwa kuweko wageni katika tume ya kusimamia uchaguzi ya Afghanistan ni dhidi ya kujitawala nchi hiyo. Uchaguzi wa rais wa Afghanistan umepangwa kufanyika Aprili 5 mwaka 2014.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO