Monday, April 22, 2013

SERIKALI YAKATAA KUMFUNGULIA KESI MUSHARRAF

 
Serikali ya Pakistan leo imekataa kumfungulia mashtaka ya uhaini, kiongozi wa zamani wa kijeshi wa nchi hiypo, Pervez Musharraf, na imeiambia Mahakama Kuu kwamba hiyo ni zaidi ya mamlaka yake. Hatua hiyo angalau itampa nafuu kidogo, Musharraf ambaye tayari yuko katika kizuizi cha nyumbani kutokana na shtaka moja kati ya matatu yanayomkabili, anayodaiwa kuyafanya akiwa madarakani kuanzia mwaka 1999 hadi mwaka 2008. Kesi hizo zinasikilizwa katika mahakama za mwanzo. Musharraf amekuwa akitishiwa kuuawa na kundi la Taliban na amezuiwa kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao. Mahakama Kuu inasikiliza ombi la mawakili wanaotaka Musharraf afunguliwe mashtaka ya uhaini kwa kukiuka katiba. Nchini Pakistan, ni serikali pekee inayoweza kumfungulia mtu kesi ya uhaini, ambayo adhabu yake ni hukumu ya kifo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO