Friday, May 03, 2013

HUKUMU YA SHEIKIH PONDA MAY 9

Kutoka AHLU SUNNAH GROUP ON FACEBOOK.


Hukumu ya Sheikh Ponda Issa Ponda (Hafidhahullah) na Waislamu wenzake 49 wiki ijayo InshaALLAH. Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu jijini Dar es Salaam imepanga Mei 9 mwaka huu, kuwa siku ya hukumu ya kesi ya Sheikh Ponda Issa Ponda (Hafidhahullah) na wenzake 49. Waislamu wengine 52 tayari wameshahukumiwa miaka mitatu jela. LAA HAULA WALAA KHUWATA ILAA BILAAH, Ndugu zetu wanateswa kwa ajili ya kusema Mola wetu ni ALLAH. May 9 mwaka tufike mahakamani kwa ajili ya Kusikiliza Hukumu ya Ndugu zetu InshaALLAH.

Dua Zetu Muhimu sana kwa Ndugu zetu Waislamu Popote walipo, 
ALLAH awape Subira Katika Mitihani hii ya Dunia ALLAH awazidishie Iman na Taqwa (Ucha Mungu) Amiin.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO