Saturday, May 04, 2013

KUONDOKA WANAJESHI WA ETHIOPIA SOMALIA

Serikali ya Ethiopia imetangaza kuwa askari wote wa jeshi la nchi hiyo wameondoka katika ardhi ya Somalia. Wanajeshi wa Ethiopia waliingia katika ardhi ya Somalia mwezi Novemba mwaka 2011 kwa lengo la kushirikiana na wanajeshi wa Kenya pamoja na vikosi vya serikali ya mpito ya Somalia katika operesheni za kuwatomeza wanamgambo wa kundi la Ash Shabab. Kwa kuondoka kundi la mwisho la wanajeshi waliokuweko katika mji wa Baidoa huko kusini magharibi mwa Somalia, kuwepo kijeshi kwa Ethiopia ndani ya ardhi ya Somalia kumefikia tamati. Hata hivyo askari wa jeshi la Kenya ambao waliingia nchini Somalia mwezi Oktoba miaka miwili iliyopita kwa madhumuni ya kuwasaka na kuwatokomeza wanamgambo wa Ash Shabab, wao wataendelea kubakia nchini humo. Baada ya kupata idhini rasmi iliyotolewa na Umoja wa Afrika mnamo mwezi Januari mwaka huu, wanajeshi wa Kenya walijiunga rasmi na operesheni ya umoja huo ya kurejesha amani nchini Somalia AMISOM. Baada ya kuondoka wanajeshi wa Ethiopia jukumu la kulinda amani na kurejesha utulivu katika mji wa Baidoa limekabidhiwa kwa vikosi vya AMISOM.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO