Saturday, May 25, 2013

ISRAEL YAONGEZA MISAADA KWA WAASI WA SYRIA

Mamia ya majeruhi ya wanamgambo wa makundi ya waasi nchini Syria wamehamishiwa kwenye hospitali za utawala wa Kizayuni wa Israel kwa minajili ya kupatiwa matibabu. Gazeti la al Manar la Palestina limeandika kuwa, kiwango cha misaada ya utawala wa Kizayuni wa Israel kwa makundi ya waasi ya Syria ni kikubwa, na kueleza kwamba utawala wa Israel unadhamini mahitajio ya kivita ya magaidi na kuwapatia huduma nyingine nyingi kwa lengo la kuongeza mashambulizi yao dhidi ya serikali ya Damascus. Gazeti la al Manar limefichua kwamba, yapata miezi saba iliyopita, utawala wa Israel ilianza  kujenga hospitali ya kijeshi katika moja ya kambi zake zilizoko katika eneo la milima ya Golan ya Syria inayokaliwa kwa mabavu na utawala wa Israel kwa minajili ya kutoa huduma za kimatibabu kwa waasi wa Syria. Hii ni katika hali ambayo, Saudi Arabia  na Qatar zimeupatia utawala wa Israel mamia ya milioni ya dola kutokana na huduma inazozitoa kwa makundi ya waasi ya Syria.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO