Friday, May 31, 2013

MAREKANI: IRAN YAONGEZA MISAADA YA KIGAIDI

Iran imeongeza msaada wake kwa makundi ya kigaidi, na nguvu za mtandao wa kigaidi wa Al-Qaida zimepungua- haya yametajwa katika ripoti ya mwaka ya Marekani, juu ya hali ya ugaidi duniani. Wizara ya mambo ya nchi za nje ya nchi hiyo imekitaja kikosi cha walinzi wa mapanduzi cha Irani, wizara ya ujasusi ya nchi hiyo na msada inaoutoa kwa kundi la wanamgambo wa kishia nchini Lebanon, Hizbollah.
Ripoti ya Marekani imesema kuwa msaada wa Iran kwa ugaidi umefika kwenye kiwango ambacho hakijaonekana tangu miaka ya 1990, ikifadhili mashambulizi katika maeneo ya kusini mashariki mwa Asia, Ulaya na Afrika.
 Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mtandao wa al-Qaida ambao kwa muda mrefu ndio ulikuwa shabaha kubwa ya vita dhidi ya ugaidi umeendelea kudhoofika baada ya kuuawa kwa viongozi wake kama Abu Yahya al-Libi na Abu Zaid al-Kuwaiti.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO