Tuesday, June 25, 2013

ASKARI 57 WA MAREKANI WAINGIA SYRIA

Duru za habari zinaarifu kuingia nchini Syria askari 57 waliostaafu wa Marekani kwa ajili ya kuwasaidia magaidi wanaotekeleza mauaji na uharibifu nchini humo. Shirika la Habari la Fars limeripoti kuwa maafisa hao 57 waliwasili nchini Uturuki na ndege ya Kimarekani ya C-130 na kuingia Syria kupitia njia ya mkoa wa mpakani wa Reyhanlı. Aidha ndege hiyo ilikuwa imebeba pia zana za kijasusi kwa ajili ya kuwasaidia magaidi. Wakati hayo yakiripotiwa, kikao cha siku ya Jumamosi cha nchi zinazojiita eti marafiki wa Syria kilichofanyika mjini Doha, Marekani na baadhi ya nchi za Magharibi ikiwemo Uturuki, Qatar na Saudia, zilikubaliana kuongeza misaada yao kwa wapinzani wa Syria na makundi ya kigaidi yenye mafungamano na kundi la kigaidi la Al-Qaida. Wakati huo huo, magaidi ambao wanaonekana kushindwa na jeshi la serikali halali ya Rais Bashar al-Assad wa nchi hiyo, wameanzisha wimbi jipya la kuwashambulia ovyo raia wasio na hatia wa nchi hiyo, ili kwa njia hiyo waweze kuishinikiza serikali ya Damascus. Weledi wa masuala ya kisiasa wa Mashariki ya Kati wanaamini kuwa, kikao cha Doha, Qatar hakikufanikiwa na kwamba, ni mwanzo wa kushindwa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO