Tuesday, June 25, 2013

SILAHA TOKA ISRAEL ZAWASILI SYRIA

Shehena ya kwanza ya silaha za kisasa zilizoundwa Israel imetumwa kwa magaidi wa Syria. Mtandao wa Intaneti ya gazeti la al Manar la Palestina umeripoti kuwa hatua ya Israel ya kutuma ya shehena ya kwanza ya silaha za kisasa kwa makundi ya kigaidi huko Syria imekuja kufuatia ombi la Washington la kuutaka utawala wa Kizayuni ufanye hivyo.
Ripoti hiyo imeongeza kuwa, ndege kadhaa za kijeshi za Israel zimesafirisha silaha hizo hadi nchini Uturuki kwa nyakati mbili tofauti na baadae silaha hizo zitapelekwa kwenye maghala maalumu ya silaha kwenye mpaka ya Uturuki na Syria na baadaye kutumwa kwa magaidi wanaofanya mauaji ndani ya ardhi ya Syria. Utawala wa Kizayuni wa Israel umetoa misaada hiyo ya kijeshi kwa magaidi wa Syria huku mfalme wa Saudi Arabia akiutaka utawala wa Kizayuni ufanye mashambulizi mengine ya anga ndani ya ardhi ya Syria.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO