Saturday, June 29, 2013

GHASIA ZAUA WAWILI MISRI

Watu wawili wameuwawa na wengine wengi wamejeruhiwa katika mji wa pili kwa ukubwa nchini Misri wa Alexandria kufuatia mapigano kati ya wafuasi na wapinzani wa rais mwenye msimamo wa itikadi kali za Kiislamu Mohammed Mursi.Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imethibitisha kwamba raia wa Marekani mwenye umri wa miaka 21 ni miongoni mwa waliouwawa.Katika mji wa Port Said pia kuna mtu mmoja aliyeuwawa na wengine wengi wakajeruhiwa baada ya kutokea mripuko katika maandamano.Polisi imesema bado haijafahamika ikiwa mripuko huo unahusiana na maandamano hayo.Maelfu ya watu wamekusanyika katika miji mbali mbali kote nchini Misri kushiriki maandamano ya kumpinga Rais Mursi huku ghasia zikiripotiwa pia katika mji mkuu wa nchi hiyo Cairo na katika mkoa wa Aga.Ghasia hizo zinashuhudiwa kabla ya  maandamano makubwa kabisa dhidi ya serikali yaliyopangwa kufanyika kesho Jumapili.Marekani imetowa tahadhari kwa raia wake kutosafiri nchini Misri wakati ikiwataka pia wafanyikazi wote katika ubalozi wake wasiokuwa na kazi za lazima kuondoka nchini humo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO