Sunday, June 30, 2013

OBAMA KUZURU GEREZA ALILOFUNGWA MANDELA

Rais Barack Obama wa Marekani ameendelea na ziara yake nchini Afrika Kusini na hii leo jumapili yeye pamoja na familia yake watatembelea kisiwa vya Robben na kuzuru gereza ambalo Rais wa zamani wa Taifa hilo na kinara wa vita dhidi ya ubaguzi wa rangi Nelson Mandela alitumikia kifungo cha miaka 18 kati ya miaka 27 aliyokaa gerezani.Akiwa nchini humo jana jumamosi kiongozi huyo alikutana na baadhi ya ndugu wa Mzee Mandela wakiwamo watoto na wajukuu zake huku akiahidi kuendelea kuwa karibu na familia hiyo katika kipindi hiki kigumu cha kumuuguza mpendwa wao ambaye bado hali ya ya afya yake imeendelea kuwa tata licha ya kukaa hospitalini kwa zaidi ya majuma matatu sasa.
Aidha Obama aliweka wazi sababu za yeye kutozuru Taifa la Kenya ambalo ni asili ya baba yake mzazi, miongoni mwa sababu zake ni pamoja na machafuko ya baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 inayomkabili Rais wa Taifa hilo Uhuru Kenyatta pamoja na naibu wake William Rutto katika mahakama ya kimataifa ya ICC. Hata hivyo kiongozi huyo ameahidi kuzuru Taifa hilo kabla ya kukamilika kwa muda wake wa Urais nchini Marekani. Akiwa katika siku ya mwisho ya ziara yake nchini Afrika Kusini Rais Obama anatarajiwa kutoa hotuba ihusuyo sera ya Marekani kwa Afrika katika chuo kikuu cha Cape Town.
Ziara ya Obama nchini Senegal, Afrika Kusini na Tanzania inalenga kubadilisha fikra zilizojengeka kuwa kiongozi huyo amekuwa akijiweka kando na maswala ya Afrika tangu kuanza kuliongoza Taifa tajiri la Marekani mwaka 2008.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO