Wednesday, June 26, 2013

JESHI LA afghanistan lazima shambulio dhidi ya ikulu

Wapiganaji wa kundi la wanamgambo wa Talibans, wameendesha shambulio dhidi ya Ikulu ya rais jijini Kaboul bila mafaanikio, baada ya majeshi ya serikali kufaulu kuzima shambulio hilo na kuwauawa washambuliaji wote. Tukio hili linajiri juma moja tu baada ya kuanzishwa kwa mchakato wa amani nchini humo na ambapo ofisi ya kisiasa ya kundi hilo, imefunguliwa jijini Doha. Mkuu wa polisi jijini Kaboul Mohammad Ayoub Salangi amesema takriban waasi wanne walioendesha shambulio hilo wameuawa, na hakuna wengine walioathirika.
Upande wake naibu mkuu wa polisi Mohammed Daud Amin amefahamisha kuwa Washambuliaji walikuwa ndani ya magari mawili tofauti huku wakibebelea mabomu ya kulipuka na kupita karibu na majengo ya Ikulu ya taifa na majengo ya shirika la kijasusi la nchini Marekani CIA, na walijaribu kujilinganisha na wanajeshi wa vikosi vya NATO nchini Afghanistani ISAF. Mohammad Daud Amin ameendelea kuwa wahalifu hao walikuwa katika magari mawili yanayo tumiwa na vikosi vya ISAF huku wakivalia sare za wanajeshi hao wakiwa na vifaa aina ya wanavyo tumia wanajeshi wa vikosi vya kujihami vya nchi za magharibi NATO nchini Afghanistani.
Magari hayo mawili yalijaribu kuvuka kituo cha uchunguzi, baada ya moja kufaulu kuvuka na nyingine kushindwa polisi ilitilia mashaka gari hilo na ndipo mapigano yakaanza na magari hayo yakalipuka. Duru kutoka ikulu ya rais nchini Afghanistani zaarifu kuwa rais wa nchi hiyo Hamid Karzai alikuwa amepanga kufanya kikao na vyombo vya habari mapema leo asubuhi. Kundi la wapiganaji wa Talibans limekiri na kujigamba kuhusika na mashambulzi hayo kupitia msemaji wake Zabihullah Mujahid ambaye amesema wanamgambo wa kundi hilo wameshambulia ofisi za CIA, ofisi za Ikulu ya rais pamoja na wizara ya ulinzi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO