Friday, June 28, 2013

KERRY ALAUMU MIPANGO YA UTAWALA WA ISRAEL

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry amesema utawala haramu wa Israel unavuka mipaka kwa kuidhinisha ujenzi wa vitongoji vipya vya walowezi wa Kizayuni.
Kerry alisema hayo baada ya kukutana na Waziri mkuu wa utawala huo ghasibu, Benjamin Netanyahu hapo jana. Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amesema Tel Aviv inafuata mkondo mbaya ambao unaendelea kuzima matumaini ya kupatikana amani Mashariki ya Kati. Amesema kwamba, kwa hali ilivyo hivi sasa, uwezekano wa kuwa na mataifa mawili kama njia ya kutatua mgogoro wa Israel na Palestina unaendelea kufifia na kwamba itafika sehemu ambapo itakuwa vigumu kabisa kwa amani ya Mashariki kupatikana.
Hii ni katika hali ambayo, Umoja wa Mataifa umesisitiza mara kadhaa kwamba ujenzi wa vitongoji vya Wazayuni katika ardhi za Wapalestina ni kinyume cha sheria za kimataifa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO