Friday, June 28, 2013

WAZIRI WA ULINZI LIBYA AFUTWA KAZI

Waziri Mkuu wa Libya Ali Zeidan amemtimua kazi Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo Mohammed al Barghathi baada ya kutokea mapigano makali mjini Tipoli baina ya makundi mawili yenye silaha ambayo yamesababisha vifo vya watu watano na kujeruhi makumi ya wengine.
Ali Zeidan amesema baada ya yaliyojiri jana imeamuliwa kwamba Waziri wa Ulinzi ataachichwa kazi. Tutatanganza waziri mpya wa ulinzi hivi karibuni, amesisitiza Waziri Mkuu wa Libya.
Uamuzi huo wa kumfuta kazi Waziri wa Ulinzi wa Libya umechukuliwa huku nchi hiyo ikusumbuliwa na mapigano ya mara kwa mara kati ya makundi ya wanamgambo wanaobeba silaha.
Jumatano iliyopita watu wengine 5 waliuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa katika mapigano makali yaliyotokea baina ya makundi hasimu kwenye wilaya ya Salahuddin. Mji wa pili kwa ukubwa nchini Libya wa Benghazi pia umekumbwa na machafuko makubwa ambapo vituo kadhaa vya polisi vimelipuliwa kwa mabomu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO