Sunday, June 30, 2013

MAANDAMANO MAKUBWA YAANZA MISRI LEO

Maandamano makubwa yameanza leo nchini Misri ambapo kuna wasi wasi wa kuibuka machafuko baina ya wafuasi na wapinzani wa Rais Mohammad Morsi.
Waandamanaji hasimu walianza kukusanyika Jumamosi usiku kwa ajili ya maandamano yanayofanyika katika kipindi hiki cha kuwadia mwaka mmoja tokea Morsi achaguliwe kuwa rais wa Misri. Watu watatu tayari wamesharipotiwa kupoteza maisha katika machafuko ya Jumamosi katika maeneo kadhaa ya Misri. Wapinzani wameitisha maandamano makubwa katika medani ya Tahrir mjini Cairo kwa lengo la kumtaka Rais Morsi ajiuzulu. Hata hivyo wafuasi wa Harakati ya Ikwanul Muslimin nao wameitisha maandamano yao wakimuunga mkono Rais Morsi. Hali hiyo imeibua wasi wasi wa uwezekano wa kuzuka machafuko na ghasia kote Misri katika maandamano ya leo. Wapinzani wanataka Rais Morsi ajiuzulu na uchaguzi wa mapema kuitishwa. Wanamlaumu kiongozi huyo kuwa amekengeuka mkondo wa mapinduzi yaliyomtimua madarakani dikteta Hosni Mubarak. Uamuzi wa Mursi wa kukata uhusiano na Syria na kuwaunga mkono magaidi nchini humo pia ni jambo ambalo limewakasirisha Wamisri.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO