Friday, June 28, 2013

MAREKANI YAONYA KUTOKEA MASHAMBULIZI ZAIDI AFGHANISTAN

Marekani imeonya juu ya kutokea kwa mashambulizi zaidi ya wanamgambo wa kundi la taliban, licha kuanzishwa kwa mchakato wa amani tangu kufunguliwa kwa ofisi za kundi hilo nchini Qatar. Wanamgamba hao wa Taliban walishambulia hivi majuzi ofisi ya rais na ile ya shirika la ujasusi la Marekani CIA jijini Kaboul na kuwauwa walinzi watatu shambuli ambalo liliashiria uzaifu wa mchakato wa amani juma moja baada ya kuzunduliwa kwa ofisi za Talibans jijini Doha.
Shambulio hilo lilioendeshwa na wapiganaji watano waliovalia nguo za wanajeshi wa Kikosi cha kujihami cha majeshi ya nchi za magharibi nchini Afghanistan Nato, ni shambulio kubwa kuwahi kufanywa na wapiganaji hao tangu mwaka 2008 wakati wa jaribio la kutaka kumuuwa rais wa nchi hiyo Hamid Karzai. Mjumbe maalum wa Marekani nchini Afghanistan na Pakistan, James Dobbins amesema katika mkutano na vyombo vya habari jijini New Delhi, huenda wapiganaji wa Taliban wakaonyesha nia ya kuzungumza huku wakionyesha kwamba wako na nguvu. Dobblins amesema kuwa wanamgambo wa Talibans wanataka kuendeleza shinikizoili ionekana kwamba Marekani wameondoka nchini Afghanistan kufuatia shinikozo kutoka kwao.
Dobbins anazuru nchini India siku kadhaa baada ya ziara ya waziri wa mambo ya nje wa Marekani nchini humo John Kerry, na kuweka wazi kwamba wamezungumza na viongozi wa Hew Delhi kuhusu kusua sua kwa mchakato wa mazungumzo ya amani nchini Afghanistan hali ambayo inazua hofu kwa viongozi wa India. Kiongozi huyo amesema viongozi wa India wanahofu, hofu ambayo watu wote wanayo, kwakuwa hakuna anaye juwa kitachotokea. Serikali ya New Delhi inahofia kurejea tena kwa utawala wa Talibans Kaboul baada ya kundoka kwa vikosi vya Nato mwaka 2014, na ambayo ilitowa dola za Marekani Bilioni mbili kama msaada kwa Afghanistan ili kukabiliana na ushawishi wa Pakistan katika kuwafadhili watu wenye msimamo mkali.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO