Friday, June 28, 2013

OBAMA HAJAZUNGUMZA NA CHINA WALA URUSI

Aliyekuwa mfanyakazi wa Shirika la Ujasusi la Marekani Edward Snowden hawezi kuondoka katika eneo alilojificha la uwanja wa ndege wa Moscow ili kusafiri kuelekea mahali kwingine kwa sababu stakabadhi zake sio halali. Chanzo cha habari kimeliambia shirika la habari la Urusi kuwa Snowden hatasafiri kuelekea Cuba au kwingineko kwa sababu hana vibali. Rais wa Marekani, Barack Obama, amesema leo kuwa hajazungumza na Rais wa China, Xi Jinping, au Rais wa Urusi, Vladmir Putin, kuhusiana na ombi la Marekani kuzitaka nchi hizo kusaidia kumrudisha nyumbani Marekani Snowden, kwa sababu hastahili kufanya hivyo. Akizungumza katika kikao cha waandishi habari nchini Senegal ambako ameanzia ziara yake ya mataifa matatu barani Afrika, Obama amesema njia za kawaida za kisheria zinatosha kutumika kuhusiana na ombi hilo la serikali ya Marekani. Amesema wana ushirikiano mkubwa na China na Marekani kuhusiana na masuala mengi na hivyo basi hawawezi kuangazia kisa cha mshukiwa mmoja tu ambaye wanajaribu kumsaka.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO