Saturday, June 29, 2013

WAFUASI WA MURSI WAANDAMANA KUMUUNGA MKONO

Makundi ya Kiislam nchini Misri yametowa wito kwa wafuasi wao kushiriki katika maandamao yasiokuwa na kikomo kuanzia leo Ijumaa, kumuunga mkono rais wa taifa hilo Mohamed Morsi, ikiwa ni siku mbili ya upinzani kukusanyika kuandamana wakimtaka rais huyo kujiuzulu baada ya kile wanachosema ameshindwa kuboresha maisha ya wananchi na kufikia malengo ya mapinduzi ya mwaka 2011 yaliomg'oa rais Hosni Mubarak Madarakani. Wafuasi wa rais Morsi wanaandamana leo siku ya Ijumaa, katika maandamano yatayo endelea na haijulikani itavyokuwa katika siku mbili zijazo kufuati upinzani nao kupanga kuandamana Juni 30. Jeshi la usalama nchini humo limeimarisha usalama jijini Cairo na miji mingine nchini humo kukabiliana na ghasia ambazo zaweza kuibuka.
Wapinzani nchini Misri wanasema wamechoka na uongozi wa rais Morsi na wanamtaka ajiuzulu baada ya mwaka mmoja wa kuwa uongozini huku wafuasi wa Morsi wakisema hawawezi kuruhusu kiongozi wao kutishwa na watu wachache. Siku ya Jumatano, maandamano yalifanyika mjini Mansoura na kusababisha vifo vya watu wawili na wengine zaidi ya mia moja kujeruhiwa. Wachambuzi wa Siasa wanasema tatizo kubwa linalochangia hali kuendelea kuwa mbaya nchini humo ni kwa sababu ya katiba ambayo imeegemea mno dini ya Kislamu.
Siku ya Jumatano rais Morsi aliadhimisha sherehe za mwaka mmoja tangu kuchukua hatamu ya uongozi nchini humo baada ya kuanguka kwa utawala wa Hosni Mubarak mwaka 2011. Rais Morsi amewaonya wananchi wa taifa hilo kuacha kuegemea mirengo ya kisiasa ili kuepuka nchi hiyo kugawanyika. Mwendelezo wa maandamano nchini humo unaelezwa na wachambuzi wa kiuchumi kuwa huenda pia ukachangia kuporomoka kwa uchumi nchini humo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO