Saturday, June 29, 2013

RAIS WA ECUADOR ATANGAZA KUFUTA MKATABA NA MAREKANI

Wakati Marekani ikiendesha vitisho na madhara kwa taifa litalo mpa hifadhi ya kisiasa mshauri wa zamani wa Kituo cha Usalama cha Marekani NSA, na mfanyakazi wa shirika la Ujasusi la Marekani Edward Snowden, Rais wa Ecuador Rafael Correa atangaza kusitisha mkataba wa mapendekezo ya ushuru uliotolewa na Marekani ikiwa ni sehemu ya mapambano dhidi ya biashara ya madawa ya kulevya. Rafael Correa ameiambia Marekani kwamba hawataki vitisho, na ndio sababu wameamuwa kufuta viwango vya ushuru vilivyo pendekezwa kwa upande wao na hawawezi kubadili hatuwa hii, hivyo kuiomba Marekani ibaki na mapendekezo yake.
Kiongozi huyo wa mrengo wa kisocialist aliechaguliwa februari iliopita kwa muhula wa miaka mitano amekuwa na uhusiano mbovu na Marekani. Makubaliano ya forodha baiba ya taifa hilo na Marekani yalianza kutumika mwaka 1991. Yalirahisisha mauzo ya mafuta Ekuador, maua, matunda kwenda kuuzwa nchini Marekani, ikiwa ni kiwango cha takriban dola za Marekani Milioni ishirini na tatu kwa mwaka. Tangu kuvijisha siri za Marekani kuwa imekuwa kwa muda mrefu ikiendesha uchunguzi wa mawasiliano ya ki elektroniki kwa mataifa mbalimbali duniani, Edward Snowden anatafutwa na serikali ya Marekani kwa kile kinacho daiwa na serikali hiyo kwamba ni uhaini.
Snowden amekwama kwenye uwanja wa ndege wa jijini Moscou akisubiri kupewa hifadhi na serikali ya Ecuador. Marekani imekuwa ikiomba Urusi kumsafirisha afisaa huyo nchini Marekani kwa ajili ya kuhojiwa na vyombo vya sheria, jambo ambalo Urusi imekuwa ikikanusha kuwepo katika ardhi yake na kuweka wazi kwamba amekwama kwenye eneo la Uwanja wa Ndege.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO