Sunday, July 28, 2013

ALIYEFUTWA KAZI SUDAN KUWANIA URAISI SUDAN

Aliyekuwa makamu wa Rais wa Sudan Kusini Riek Machar amesema atagombea urais katika uchaguzi mkuu mwaka 2015 dhidi ya Rais Salva Kiir aliyemfuta kazi mapema wiki hii. Akizungumza katika mkutano wa hadhara jana kwa mara ya kwanza tangu kufutwa kazi, Machar alisema atawania kupitia chama tawala na kumpinga Kiir. Machar ameongeza kuwa ili taifa hilo liungane haliwezi kuvumilia utawala wa kiimla.Rais Kiir alivunjilia mbali baraza la mawaziri na kumfuta kazi makamu wake siku ya Jumanne kufuatia ripoti kuwa kuna mzozo wa uongozi ndani ya chama tawala hasa kati ya Kiir na Machar.Kiir amepunguza idadi ya mawaziri kutoka 29 hadi 18. Pia alimsimamisha kazi katibu mkuu wa chama cha SPLM Pagan Amum akisubiri kukamilika kwa uchunguzi wa madai ya kudharau mamlaka na kuleta mgawanyiko ndani ya chama tawala. Machar amesema Kiir ana haki kikatiba kumfuta kazi makamu wa rais na kulivunja baraza la mawaziri lakini amemshutumu kwa kile alichokiita pengo la uongozi lilioachwa baada ya hatua hiyo kwa kushindwa kujaza nafasi zao mara moja.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO