Sunday, July 28, 2013

MAZUNGUMZO KATI YA ISRAEL NA PALESTINA KUANZA JUMANNE

Wapatanishi wa Israel na Palestina watakutana mjini Washington Marekani Jumanne ijayo kufufua  mazungumzo ambayo yalikuwa yamekwama kwa miaka mitatu. Afisa mmoja wa wapalestina ambaye hakutaka jina lake kutajwa ameliambia shrika la habari la Afp kuwa ujumbe wa Palestina utaongozwa na  Saeb Erakat huku ule wa Israel ukiongozwa na waziri wa sheria Tzipi Livni na kuongeza kuwa maafisa wa Marekani pia watashiriki. Waziri wa maendeleo ya kanda wa Israel Silvan Shalom mapema wiki hii alisema mazungumzo hayo yataanza Jumanne lakini haikuwa imethibitishwa tarehe hiyo wala mahali watakapokutana. Mjumbe mkuu wa Israel Livni ataandamana na balozi wa kibinafsi wa waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu Yitzhak Molcho.Kulingana  na maafisa wakuu wa Israel agenda kuu ya mkutano huo wa washington itakuwa juu ya jinsi ya kufanya mazungumzo hayo na pia  mada zitakazojadiliwa pamoja na ratiba yake.Kituo cha redio nchini humo kimesema leo wafungwa zaidi ya 100 wanatarajiwa kuachiliwa huru katika kipindi cha mazungumzo hayo ambayo yanatarajiwa kudumu kwa kati ya miezi sita na tisa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO