Thursday, July 18, 2013

DHAMBI KUBWA YA WANAWAKE WANAOJIFANANISHA KIUME NA WANAUME WANAOJIFANANISHA KIKE.

Mwenyezi Mungu S.W.T. amewalani wanawake wanaojifananisha kiume na wanaume wanaojifananisha kike, na ndio maana ikawa ni katika madhambi makubwa sabini. Mfano wa kujifananisha ni kama vile: Kuzungumza, kutembea, kuvaa mavazi; na kwa wanawake, kumpenda mwanamke mwingine kama wanaume kwa ajili ya kusagana wanawake kwa wanawake (Lesbians), na kwa wanaume, ni kuingiliana wanaume kwa wanaume (Homosexuals). Kutokana na maumbile ya Mwenyezi Mungu S.W.T. ameumba wanaume na ameumba wanawake, na tabia zao na mavazi yao na msemo wao ni tofauti kabisa, lakini ikiwa mwanamume atajifananisha kuwa sawa na mwanamke au mwanamke kuwa sawa na mwanamume, basi watakuwa wamezibadili wao wenyewe taratibu walizopangiwa na kuwekewa na Mola wao, na kwahivyo watakuwa wametenda dhambi kubwa. Mtume S.A.W. kasema katika Hadithi iliyotolewa na L-Bukhari, “

‘‘لَعَنَ الله الْمُتَشَبِّهَاتِ مِنَ النِّسَاءِ بِالرِّجَالِ وَالْمُتَشَبِّهِينَ مِنَ الرِّجَالِ بِالنِّسَاءِ’’

Maana yake, “Wamelaaniwa na Mwenyezi Mungu wanaojifananisha wanawake kiume na wanaojifananisha wanaume kike.” 
Pia Mtume S.A.W. kasema katika Hadithi nyingine iliyopokelewa na Ibn Abbaas R.A.A. na kutolewa na Abu Daud, “

‘‘لَعَنَ اللَّه الْمُخَنَّثِينَ مِنَ الرِّجَالِ وَالْمُتَرَجِّلاتِ مِنَ النِّسَاءِ’’

Maana yake, “Mwenyezi Mungu amewalani wanaume wanaojifananisha kike na wanawake wanaojifananisha kiume.” 
Na pia Mtume S.A.W. kasema Hadithi iliyopokelewa na Abu Huraira R.A.A. na kutolewa na L-Bukhari, “

‘‘لَعَنَ اللَّه المرأة تلبس لبسة الرِّجَالِ والرِّجَالِ يلبس لبسة المرأة’’

Maana yake, “Mwenyezi Mungu amemlani mwanamke anaevaa mavazi ya kiume na mwanamume anaevaa mavazi ya kike.” 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO