Friday, July 26, 2013

HANIA ALAANI PROPAGANDA ZA WAARABU

Waziri Mkuu wa serikali halali iliyochaguliwa na wananchi ya Palestina amelaani vikali propaganda za baadhi ya vyombo vya habari vya Kiarabu dhidi ya taifa la Palestina. Taarifa iliyotolewa na ofisi ya Waziri Mkuu, Ismail Hania, sambamba na kulaani propaganda hizo zinazofanywa na baadhi ya vyombo vya habari vya nchi za Kiarabu imetangaza kuwa, madai ya vyombo hivyo vya habari kwamba, Wapalestina na Muqawama wa Palestina ulikuwa na nafasi katika matukio ya Misri ni uongo wa wazi ambao ni kwa maslahi ya utawala haramu wa Israel. Wakati huo huo, Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imelaani hukumu ya mahakama moja nchini Misri ya kuendelea kumshikilia Muhammad Mursi, Rais aliyeondolewa madarakani nchini humo kwa tuhuma za kushirikiana na harakati ya Hamas ya Palestina. Sami Abu Zuhri, msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema, maana ya uamuzi huo ni kuwa harakati hiyo ni adui wa taifa la Misri.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO