Friday, July 26, 2013

UN YALAANI SERA ZA ISRAEL KUCHUKUA ARDHI ZA PALESTINA

Navi Pillay Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ameutaka utawala wa Kizayuni wa Israel kuufanyia mabadiliko mswada wa sheria ambao ikiwa utatekelezwa utasababisha kuporwa kwa ardhi katika eneo la Negev na hivyo kupelekea watu takribani 40,000 kutoka jamii ya Bedouin kutimuliwa kutoka kwenye ardhi ya mababu zao.
Pillay anasema kuwa 'watu wa jamii ya Bedouin wana haki sawa ya kumiliki mali, nyumba na kupata huduma za umma kama jamii nyingine yeyote ile ya Israel'. Pillay alielezea masikikitiko yake kuwa bado utawala wa Israel unaendelea kuwalazimu watu wenye asili ya Kiarabu kuhama makwao hata baada ya kulizungumzia suala hilo alipofanya ziara Israel miaka miwili iliyopita. Pillay ameongeza kuwa ikiwa mswada huo utakuwa sheria utachochea kubomolewa kwa makao ya jamii hiyo na kuwalazimu watu hao kuhama makwao hatua ambayo itawanyima haki yao ya kumiliki ardhi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO