Friday, July 26, 2013

JESHI HISPANIA LAMHOJI DEREVA WA TRENI ILIYOPATA AJALI

Jeshi la Polisi nchini Uhispani linatarajiwa kuanza kumhoji mmoja wa madereva wa garimoshi lililopata ajali nchini humo na kuchangia vifo vya abiria wanaokadiriwa kufikia themanini na kuwaacha wengine zaidi ya mia moja thelathini wakijeruhiwa. Jeshi limesema kuwa mahojiano hayo ni sehemu ya uchunguzi ulianza kufanyika kubaini chanzo cha ajali hiyo mbaya zaidi ya garimoshi kutokea katika kipindi cha miaka 40 nchini humo. Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi imesema miongoni mwa vitu ambavyo watahitaji kujiridhisha navyo ni pamoja na kufanya uhakiki ili kujua kama kweli kama garimoshi hilo lilikuwa kwenye mwendokasi mara mbili ya uliopaswa. Vyombo vya Habari nchini Uhispania viliandika moja ya chanzo cha kutokea kwa ajali hiyo ni mwendo kasi mara mbili iliyokuwa inaenda na kuchangia kutoka kwenye njia yake ya reli kabla ya kupata ajali hiyo.
Shirika la Reli la Taifa nchini Uhispania linalotambulika kwa jina la Renfe limeweka wazi ni mapema sana kusema mwendo kasi ni chanzo cha ajali hiyo mbaya katika taifa hilo na hivyo uchunguzi wa kina unapaswa kufanyika. Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Usafirishaji nchini Uhispania Rafael Catala amesisitiza dalili za awali zinathibitsha mwendeo kasi unaweza ukawa ulichangia ajali hiyo kwa mujibu wa picha za CCTV zilizorekodi tukio hilo. Mfalme wa Uhispania Juan Cralos amewatembelea majeruhi wa ajali hiyo ya garimoshi na kusema wananchi wanapaswa kuungana kipindi hiki ambacho uchunguzi unafanywa kubaini sababu ya janga hilo la kitaifa.
Mfalme Carlos amekiri kila mwananchi wa Uhispania ameumizwa na ajali hiyo iliyotokea katika Jiji la Santiago de Compostela na hivyo huu si wakati wa kuanza kunyosheana vidole vya lawama. Waziri Mkuu Mariano Rajoy ameteua tume mbili ambazo zinajukumu la kufanya uchunguzi kubaini sababu za kutokea kwa ajali hiyo huku pia akitangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO