Saturday, July 20, 2013

MAANDAMANO MAKUBWA KUPINGA KESI YA ZIMMERMAN

Zaidi ya maandamano 100 yamepangwa nchini Marekani hii leo kwa kile waandalizi wamesema ni kutafuta haki kwa Trayvon kijana mweusi aliyeuawa na George Zimmerman.
Waandamanaji hao wanataka Zimmerman akabiliwe na mashitaka ya ukiukaji wa haki wiki moja baada ya mahakama kutompata na hatia ya kifo cha kijana ambaye hakuwa na silaha Trayvon Martin.Mamake Trayvon na kaka yake wanatarajiwa kushiriki katika maandamano ya Newyork huku babake akishiriki mjini Miami.Kuondolewa kwa mashitaka yote yaliyokuwa yakimkabili Zimmerman na mahakama ya Florida yalizua ghadhabu kote nchini Marekani miongoni mwa wamarekani weusi na kuzua mjadala wa ubaguzi wa rangi.Rais wa Marekani Barrack Obama hapo jana aliizungumzia kesi hiyo kwa mara ya kwanza akisema Trayvon Martin  huenda  angeliweza kuwa yeye miaka 35 iliyopita

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO