Thursday, July 25, 2013

WAASI SYRIA WAKIRI KUPATA PIGO KUBWA

Kamanda wa kundi la waasi nchini Syria amekiri kwamba jeshi la serikali ya Syria limepiga hatua kubwa katika kuyakomboa maeneo mbalimbali yaliyokuwa yakidhibitiwa na waasi hao nchini humo. Salim Idriss kamanda wa kikundi kinachojiita "Jeshi la Ukombozi wa Syria' amesema leo kuwa, makundi ya waasi yamevunjwa moyo na msimamo wa nchi za Ulaya na Marekani, wa kukataa kutuma silaha kwa makundi ya waasi na magaidi nchini Syria na kusisitiza kuwa, suala hilo limepelekea jeshi la Syria kusonga mbele na kuyakomboa maeneo mengi nchini humo. Kamanda wa kundi la kigaidi la Jeshi la Ukombozi wa Syria amezikosoa siasa za kindumakuwili za nchi za Magharibi na Marekani kwa kushindwa kutekeleza ahadi zao za kuwapelekea silaha waasi wa Syria. Inafaa kuashiria hapa kuwa, Uingereza  ilikuwa mstari wa mbele kuzishawishi nchi nyingine za Ulaya kuwapelekea silaha waasi na magaidi wa Syria, lakini mkakati huo ulifeli baada ya makamanda wa jeshi la Uingereza kumuonya David Cameron Waziri Mkuu wa Uingereza.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO