Friday, August 09, 2013

ALSHABAB YAWAACHILIA WAKENYA

Siku mbili baada ya kuachiliwa huru na wapiganaji wa kiislamu wa Al Shabab, Yese Mule na Fredrick Wainana, hatimaye wamekutana na familia zao.Wawili hao wamekuwa chini ya ulinzi wa maafisa wa usalama wa Kenya. Maafisa hao wawili wa serikali, walitekwa nyara zaidi ya mwaka mmoja na nusu uliopita wakati waasi walishambulia kituo cha polisi katika eneo la Wajir, Kaskazini mwa Kenya.Mule aliambia BBC kuwa walihamishwa kutoka sehemu moja hadi nyingine mara 19 huku wakiwa wamefungwa kwa minyororo na kufumbw macho wakiwa nchini Somalia wakati wote walipokuwa wametekwa nyara. Serikali ya Kenya imekanusha madai kuwa ililipa kikombozi kwa wawili hao kuachiliwa.
Al-Shabab limewateka nyara raia wa kigeni ikiwemo aliyekuwa jasusi wa Ufaransa Denis Allex aliyeuawa mwezi Januari baada ya njama ya kumuokoa kutibuka mwezi mapema mwaka huu. Bwana Mule na mwenzake Wainana, walitekwa nyara miezi mitatu baada ya jeshi la Kenya kuingia nchini Somalia kusaidia nchi hiyo kupambana na kundi la Al Shabaab. Wanajeshi wake ni sehemu ya kikosi cha muungano wa Afrika kinachosaidia serikali ya Somalia inayoungwa mkono na umoja wa mataifa dhidi ya Al shabaab.
Bwana Mule alikuwa afisaa wa wilaya ya Garisa wakati bwana Wainana akiwa karani wa serikali walipotekwa nyara na karibu wapiganaji 100 wa al-Shabab katika kambi ya polisi eneo la Gerille, mji unaopakana na Somalia. Wakenya wanane waliuawa wakati wa utekaji nayara huo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO