Friday, August 09, 2013

WITO WATOLEWA KWA MISRI

Marekani na Muungano wa Ulaya wamezitaka pande zote katika mgogoro wa kisiasa wa Misri, kumaliza mzozo wao unaosemekana kuwa hatari kwa taifa hilo. Hii ni baada ya serikali ya mpito kusema kuwa juhudi za mapatano zimekosa kufua dafu.Katika taarifa yao ya pamoja, walisema kuwa serikali ya Misri ndio ina jukumu kubwa kuanzisha mazungumzo na kuhakikisha kuwa mchakato huo unafanikiwa. Serikali ya mpito inayoungwa mkono na Jeshi, imesema kuwa jeshi litalazimika kuvunja mkusanyiko wa wafuasi wa Morsi ambao wamepiga kambi mjini Cairo wakitaka aachiliwe.
Mamia ya watu wamefariki tangu kuanza kwa vurugu zilizofuata kuondolewa mamlakani kwa Morsi tarehe 3 mwezi Julai. Tangu hapo, wanadiplomasia kutoka Marekani, Muungano wa Ulaya na Milki za kiarabu, wote wamejaribu kusuluhisha mgogoro huo. Lakini siku ya Jumatano rais wa mpito Adly Mansour alitangaza kuwa juhudi za kidiplomasia zimekosa kufaulu na hivyo kusema kuwa mazungumzo yaliisha hiyo jana.
''Juhudi hizi hazijaweza kuafikia lolote,'' ilisema taarifa ya rais. Rais alisema kuwa analilaumu vuguvugu la Muslim Brotherhood ambalo linamuunga mkono Morsi kwa kuwa sababu ya kukosa kufaulu kwa mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO