Friday, August 09, 2013

JANGA LA KIBINADAMU LAINYEMELEA GAZA

Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS Fawzi Barhoum amesema kuwa, eneo la Ukanda wa Gaza ambalo linakabiliwa na mzingiro, linanyemelewa na janga la kibinaadamu. Afisa huyo mwandamizi wa Chama cha Hamas ametahadharisha kwamba, hali ya kibinaadamu huko Gaza ni mbaya mno na kuna uwezekano wa eneo hilo kukumbwa na maafa ya kibinaadamu.  Amesema kuwa, kushadidi mzingiro huo unaofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza na kufungwa vivuko vya kuelekea katika eneo hilo, kikiwemo kivuko cha Rafah kinachopakana na Misri kumelifanya eneo hilo kukabiliwa na hali mbaya mno huku wakazi wa eneo hilo wakishindwa kujidhaminia baadhi ya mahitaji yao muhimu kama chakula. Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS ametahadharisha kwamba, endapo hakutachukuliwa hatua za haraka za kuhitimisha mzingiro huo, basi yamkini eneo la Ukanda wa Gaza likakabiliwa na maafa ya kibinaadamu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO