Saturday, August 17, 2013

JINA LINALOONGOZA UINGEREZA

Jina la Mtume wa Uislamu, Muhammad (saw) limeongoza kwa kupewa idadi kubwa zaidi ya watoto wa kiume waliozaliwa katika mji mkuu wa Uingereza, London katika mwaka 2012. Jina hilo tukufu limeshika nafasi ya pili kwa kupewa watoto wa kiume waliozaliwa nchini kote Uingereza baada ya jina la Harry.
Idara ya Takwimu ya Taifa yaUingereza imesema jina la Muhammad ndilo lililoongoza kwa kupewa watoto wengi zaidi wa kiume waliozaliwa mjini London katika mwaka uliopita wa 2012. Taarifa ya idara hiyo imesema jina tukufu la Muhammad limetolewa na wazazi kwa watoto elfu 7 na 139 wa kiume waliozaliwa mwaka jana. Jina la Muhammad pia lilisajiliwa kati ya majina mia moja yaliyoongoza mwaka jana katika mji mkuu wa Ufaransa, Paris na lilipendelewa zaidi na watu katika mji wa Marselle, na Vilevile Oslo nchini Norway.

1 comment:

  1. wanasema kwa kuwa uingereza waislam wengi.

    ReplyDelete

TUPE MAWAZO YAKO