Saturday, August 17, 2013

KATIBU WA UMOJA WA MATAIFA AKOSOA SIASA ZA ISRAEL

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  amesema kwamba siasa za ujenzi wa vitongoji vya walowezi za  utawala wa Kizayuni wa Israel zinadhoofisha  jitihada za amani zinazofanywa na jamii ya kimataifa. Ban Ki Moon amesema hayo alipotembelea Ukingo wa Magharibi hapo jana katika mkutano na waandishi habari pamoja na Mahmoud Abbas Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina. Katibu Mkuu wa Umoja wa Matiafa ameeleza kusikitishwa mno na hatua ya Israel ya kuendelea kujenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni huko Ukingo wa Magharibi likiwemo eneo la Baitul Muqaddas Mashariki.  Utawala wa Kizayuni wa Israel umejenga vitongoji vingi katika maeneo ya Palestina na kuyafanya makaazi ya walowezi wa Kizayuni suala ambalo ni kinyume cha maazimio ya kimataifa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO