Sunday, August 18, 2013

KESI YA HOSNI MUBARAK YAAHIRISHWA TENA

Kesi ya mauaji dhidi ya waandamanaji nchini Misri inayo mkabili rais wa zamani wa taifa hilo Hosni Mubarak imeahirishwa tena hapo jana Jumamosi hadi Agosti 25 baada ya kusikilizwa kwa muda mfupi jijini Cairo. Rais huyo wa zamani mwenuye umri wa miaka 85 ambaye utawala wake uliangushwa tangu mwaka 2011 baada ya kutokea maandano ya wananchi hakuwepo mahakamani wakati wa kuskilizwa kesi hiyo. Hayo yanjiri wakati Chama cha Muslim Bradherhood kimetowa wito kwa wafuasi wake kumiminika kwa wingi leo jumapili kuendeleza harakati za maandamano kuishinikiza serikali ya mapinduzi ilipo kuurejesha utawala wa rais Mohamed Morsi.
Hapo jana vikosi vya polisi vilifaulu kuwatia nguvuni watu 385 wafuasi wa kiongozi huyo alieondolewa madarakani waliokwua wamejificha katika muskiti wa Al Fath jijini Cairo kwa kuhofia kutokea mauaji baada ya vurugu za siku chache zilizo gharimu maisha wa watu 750. Wafuasi hao wa Mohamed Morsi aliepinduliwa na jeshi Julay 3 mwaka huu , wametowa wito kwa mara nyingine tena kuendelea kuandamana. Hata hivyo harakati za maandamao zimeonekana kupungua kasi baada ya hapo jana katika maeneo kadhaa kushuhudiwa utulivu licha ya mikusanyiko ilioonekana jana usiku.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO