Saturday, August 17, 2013

200 WAHOFIWA KUFA UFILIPINO

Waokoaji nchini Ufilipino wanaendelea kuwatafuta zaidi ya watu 200 wasiojulikana walipo, baada ya feri iliyokuwa imefurika abiria kugongana  na meli ya mizigo wakati wa usiku na kuzama papo kwa hapo. Miili 31 imeopolewa, lakini watu wengine 213 bado hawajulikani walipo, kwa mujibu wa idara ya ulinzi wa mwambao, ambayo imeonya kuwa idadi ya vifo huenda ikaongezeka.
Ajali hiyo ilitokea majira ya saa tatu za usiku, na mashuhuda walisema walisikia kishindo kikubwa, na kwamba ndani ya dakika kumi, feri hiyo ilikuwa itayari imezama. Watoto wachanga 58 walikuwa miongoni mwa abiria wa feri hiyo na haijajulikana ni wangapi kati yao wameokolewa. Usafiri wa feri ni maarufu sana katika taifa hilo lililo na visiwa zaidi ya 7,100, na unatumiwa hususani na watu wenye kipato cha chini wasio na uwezo wa kutumia usafiri wa ndege. Wakati ajali hiyo ilipotokea feri hiyo ilikuwa na abiria 870 wakiwemo wafanyakazi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO