Monday, August 19, 2013

KIONGOZI MWANDAMIZI WA HAMAS ASEMA ABBAS SI KIONGOZI WA WAPALESTINA

Mahmoud al Zahar, kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema wananchi wa Palestina hawakumtuma Mahmoud Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani akafanye mazungumzo na utawala wa Kizayuni wa Israel. Akizungumza na kanali ya televisheni ya al Manar Al Zahar, mbali na kusisitiza kuwa mazungumzo ya mapatano na utawala wa Kizayuni hayana maana yoyote amesema Mahmoud Abbas hawezi kuwa mwakilishi mzuri kwa ajili ya wananchi wa Palestina kwa sababu hawezi kutetea haki za Palestina. Akijibu suali la madai kwamba HAMAS imeacha mapambano na muqawama dhidi ya utawala ghasibu wa Israel Mahmoud al Zahar amesema HAMAS ingali imeshikamana na msimamo wake wa muqawama na ukombozi wa ardhi za Palestina na inawaheshimu wale wote walioikubali fikra ya muqawama. Afisa huyo mwandamizi wa HAMAS ametoa wito pia wa kutekelezwa makubaliano ya maridhiano ya kitaifa ya Palestina. Makubaliano ya maridhiano ya kitaifa baina ya Wapalestina yalisainiwa rasmi miaka miwili nyuma mjini Cairo Misri kati ya HAMAS na harakati ya Fat-h inayoongozwa na Mahmoud Abbas lakini hadi sasa hayajatekelezwa kutokana na pingamizi na ukwamishaji unaofanywa na Mamlaka ya Ndani ya Palestina

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO