Wednesday, August 07, 2013

LIBYA YAONYA JUU YA USHAMBULIAJI WA VITUO VYA AFYA

Wizara ya Afya nchini Libya imeonya juu ya kile ilichokiita kuwa ni kukaririwa mashambulizi dhidi ya hospitali na vituo vya afya nchini humo. Wizara hiyo imetoa taarifa hiyo mapema leo sambamba na kuonya kuhusiana na mashambulizi dhidi ya hospitali na vituo vya afya vya nchi hiyo, hususan mjini Benghazi na kusisitiza kuwa, mashambulizi hayo yanayofanywa na watu wanaojichukulia sheria mkononi, yana lengo la kudhoofisha huduma za sekta hiyo muhimu. Ripoti hiyo imesisitiza kuwa, kushambuliwa vituo vya afya kunahatarisha zaidi sekta hiyo na kuzitaka taasisi zote na sekta tofauti za serikali na kijamii nchini humo hasa jeshi na asasi za usalama na mabaraza yote ya mikoa kufanya juhudi kubwa ili kumaliza kadhia hiyo.
Wizara hiyo ya afya ya Libya pia imeonya juu ya mwendelezo wa vitendo hivyo na kusisitiza kuwa, kuendelea hali hiyo kunaathiri vibaya sekta ya afya, suala ambalo pia linawalazimisha madaktari na wauguzi wa Libya kukimbia maeneo yao ya kazi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO