Wednesday, August 07, 2013

MAREKANI YAFUNGA BALOZI NYINGINE 4 AFRIKA

Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani imeendelea kuchukua hatua za tahadhari kwa kufunga balozi zake nyingine 4 za Kiafrika. Hatua hiyo ya Marekani imechukuliwa kabla ya kumbukumbu ya kutimia miaka 15 tangu baada ya milipuko ya mabomu katika balozi zake huko Nairobi na Dar es Salaam tarehe 7 Agosti, 1998.
Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani imeeleza kuwa, balozi za Marekani katika nchi za Tanzania na Kenya zitaendelea kuwa wazi, isipokuwa imezifunga balozi zilizoko Rwanda, Burundi, Madagascar na Mauritius. Kabla ya hapo, Marekani ilikuwa tayari imeshatangaza kuzifunga balozi za nchi hiyo huko Misri, Jordan, Yemen, Saudi Arabia na Kuwait hadi kufikia tarehe 10 Agosti.
Duru za habari zinasema kuwa, Marekani imeamua kufunga balozi zake kutokana na wasiwasi wa kutokea mashambulio ya kigaidi ya kundi la al Qaeda katika eneo la Mashariki ya Kati, Kaskazini mwa Afrika na maeneo mengine duniani.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO