Thursday, August 15, 2013

MACHAFUKO YA MISRI NI FAIDA KWA MAREKANI NA ISRAEL

Mbunge mmoja wa ngazi za juu wa Iran amesema hali ya hivi sasa ya ghasia Misri ni kwa maslahi ya Marekani na Utawala wa Kizayuni wa Israel. Bw. Allaudin Burujerdi mkuu wa Kamati ya Usalama wa Taifa na Sera za Kigeni katika Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amelaani vikali pia mauaji ya raia nchini Misri. Ameongeza kuwa ni jambo la kusikitisha kuona nchi muhimu ya Kiislamu kama Misri ikitumbukia katika hali kama hii baada ya harakati ya kimapinduzi ya wananchi ambao waliuondoa utawala wa kidikteta. Burujerdi amesema, baada ya Wamisiri kuutimua madarakani utawala kibaraka wa Hosni Mubarak, hivi sasa Marekani na Utawala wa Kizayuni zinachochea machafuko Misri na jambo hilo linatia wasi wasi kwani yamkini nchi hiyo ikatumbukia katika vita vya ndani baina ya serikali ya mpito na harakati ya Ikhwanul Muslimin. Mbunge huyo mwandamizi wa Iran ametoa wito kwa wanasiasa, wasomi na wanazuoni Misri kutumia busara ili kuiondoa nchi hiyo katika mgogoro wa sasa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO