Thursday, August 15, 2013

HIZBULLAH YATHIBITISHA KUWASHAMBULIA WANAJESHI WA ISRAEL

Harakati ya Hizbullah imesema ndiyo iliyohusika na milipuko iliyowajeruhi wanajeshi wanne wa utawala haramu wa Israel ambao walikuwa wamepenya na kuingia kusini mwa Lebanon.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na kanali ya televisheni ya al-Mayadeen yenye makao yake Beirut, Katibu Mkuu wa Hizbullah Sayyed Hassan Nasrullah amesema Hizbullah haitauruhusu utawala haramu wa Israel ukiuke ardhi ya Lebanon.
Ikumbukwe kuwa mnamo Agosti 7 milipuko miwili iliwajeruhi wanajeshi vamizi wa Israel ambao walikuwa wameingia mita 400 ndani ya ardhi ya Lebanon katika eneo la kusini. Sayyed Nasrallah amesema, ‘Hizbullah ilikuwa na taarifa za mapema kuwa wanajeshi wa Israel walikuwa wamepanga kuingia kusini mwa Lebanon na hivyo harakati hiyo ilitega mabomu ambayo yalilipuliwa kutokea mbali wakati wanajeshi hao wa Israel walipofika hapo.’ Kufuatia milipuko hiyo jeshi la Lebanon lilitoa taarifa na kusema uingiaji huo wa askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel ni ‘ukiukaji wa mamlaka ya Lebanon’.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO