Thursday, August 15, 2013

MAKAO MAKUU YA GAVANA NCHINI MISRI YACHOMWA MOTO

Rais Barack Obama  wa  Marekani  ametoa  taarifa kuhusiana  na  hali  nchini  Misri  baada  ya jeshi  nchini humo  kuwaondoa  kwa  nguvu  waandamanaji  mjini  Cairo jana. Obama  amesema  kuwa  anasitisha  ushirikiano  wa kijeshi ambapo  majeshi  ya  nchi  hizo  yalitarajiwa kufanya  mazoezi  ya  pamoja  mwezi  huu. Pia Obama amesema Wamisri  hawapaswi  kuilaumu Marekani kwa kile  kinachotokea  nchini  humo.
Wakati huo  huo waandamanaji  kutoka makundi  ya Kiislamu  nchini  Misri wamevamia  makao  makuu  ya gavana  mjini  Cairo  leo na kuchoma  moto jengo hilo. Kituo cha binafsi cha televisheni cha CBC kimeonesha picha za makao makuu hayo yakiwaka moto wakati  wazima moto wakijaribu kuuzima moto huo.
Nao maafisa  nchini  Misri  wamesema kuwa  idadi  ya  watu waliouawa  katika mapambano  kati  ya  polisi  na waandamanaji wanaomuunga  mkono  rais aliyeondolewa madarakani  Mohammed Mursi  imefikia  zaidi ya watu 525.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO