Thursday, August 15, 2013

CAIRO KIMYA BAADA YA VIFO

Mji mkuu wa Misri Cairo umeripotiwa kuwa kimya, baada ya operesheni ya kinyama dhidi ya waandamanaji wanaomuunga mkono rais aliyepinduliwa Mohammed Morsi kupelekea vifo vya mamia ya raia. Mauaji hayo yamezua shutuma kutoka jamii ya kimataifa. Zaidi ya watu 278 waliuwawa wakati maafisa wa usalama waliposhambulia kambi mbili za wafuasi wa Bwana Morsi. Kambi hizo zilianzishwa mwezi uliopita kupinga hatua ya jeshi kumng'oa rais huyo anayezingatia itikadi za kiislamu. Hali ya hatari imetangazwa na amri ya kutotoka nje nyakati za usiku kutolewa katika miji mikuu ya Misri. Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa marekani John Kerry amesema matukio ''mabaya'' yaliyotokea ni ''pigo kubwa kwa juhudi za maridhiano''.
Afisa wa mashauri ya kigeni katika Muungano wa Ulaya, EU, Catherine Ashton na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon kadhalika wamekosoa hatua ya maafisa wa usalama kutumia nguvu dhidi ya raia.
Raia wa Misri wanaamkia siku nyingine yenye shaka juu ya mustakabal wao, anasema mwandishi wa BBC Bethany Bell aliyepo mjini Cairo. Hata baada ya amri ya kutotoka nje kuondolewa Alhamisi asubuhi, kumekuwa na magari machache katika barabara za katikati mwa Cairo na madaraja yanayovuka mto Nile, anasema mwandishi wetu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO